RAIS – AKUTANA NA WAZIRI WA NISHATI NA MIGODI WA ALGERIA

Posted by Bernard James on 4:42 AM with No comments
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Mhe. Youcef Yousif aliyemtembelea Ikulu Dar es salaam Leo Januari 7, 2014 algeria2 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya Pamoja na Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Youcef Yousif pamoja na ujumbe wake, pamoja na Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania Profesa Sospter Muhongo Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe Steven Masele na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini  Mhe E. maswi  ugemi huo ulipomtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Januari 7, 2014. algeria3 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Mhe. Youcef Yousif aliyemtembelea Ikulu Dar es salaam leo Januari 7, 2014 algeria4 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya Pamoja na Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Youcef Yousif pamoja na ujumbe wake, pamoja na Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania Profesa Sospter Muhongo Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe Steven Masele na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini  Mhe E. maswi  ugemi huo ulipomtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Januari 7, 2014. algeria5 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Mhe. Youcef Yousif aliyemtembelea Ikulu Dar es salaam leo Januari7, 2014.
……………………………………………………………………….
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumanne, Januari 7, 2014, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Nishati na  Migodi  wa Algeria Mheshimiwa  Youcef Yousfi ambaye yuko katika ziara ya siku sita nchini.
Katika ziara hii, Mheshimiwa Yousfi na ujumbe wake unaojumuisha viongozi wa mashirika ya umma, wanatarajia kutembelea kituo cha umeme cha Gridi ya Taifa cha Ubungo mjini Dar es Salaam, ujenzi wa bomba la gesi katika eneo la Vikindu na Mkuranga mkoani Pwani, machimbo ya Mererani  na Minjingu mkoani Manyara.
Rais Kikwete ameeleza kufurahishwa kwake na ziara hiyo, akisisitiza kwamba Tanzania na Algeria zimekuwa marafiki na washirikia wa karibu wa siku nyingi katika masuala ya siasa na uchumi, kufuatia  misingi imara iliyowekwa na waasisi wa nchi hizo – Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mheshimiwa Ahmed Ben Bella,
Rais amebainisha kwamba ushirikiano wa nchi hizi mbili  ni muhimu sana sio tu katika kuendeleza uhusiano wao wa  muda mrefu, bali pia katika  uwekezaji na utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi pamoja na uendelezaji wa rasilimali watu.